Friday, March 23, 2012
IFAHAMU SIMBA SPORT CLUB
SIMBA SC: Imetoka wapi?
NCHINI Tanzania, Simba ni jina kubwa kuliko kinywaji cha Cocacola. Ni miongoni mwa timu mbili zenye washabiki wengi zaidi si tu nchini humu, lakini katika ukanda mzima wa Afrika Mashariki.
Ina majina mbalimbali ya utani kama vile Wekundu wa Msimbazi na Lunyasi na ina makao yake makuu katika mtaa wa Msimbazi jijini Dar es Salaam.
Timu hii ilianzishwa mwaka 1936 jijini Dar es Salaam ikitumia jina la Queens lakini baadaye lilibadilisha jina na kuitwa Eagle kabla ya kubadilishwa tena na kuitwa Sunderland –jina lililotumika hadi mwaka 1971 ambapo ndipo jina la Simba Sports Club lilianza kutumika.
Ingawa tayari jina la Sunderland lilikuwa maarufu na kubwa tayari, lilibadilishwa na kuwa Simba; jina la mfalme wa msituni, ikiwa ni kutokana na pendekezo la aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Hayati Sheikh Abeid Amani Karume, ambaye alishauri jina libadilishwe wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la makao makuu ya klabu mtaa wa Msimbazi.
Katika majina yaliyopendekezwa, jina la Simba lilikubaliwa zaidi na wengi na likaamuliwa kutumika kuanzia mwaka huo wa 1971.
Simba ilianza kutanuka zaidi wakati ikitumia jina la Sunderland. Ilikuwa na matawi yake katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam ambapo ziliundwa timu zilizokuwa na kazi ya kupika wachezaji waliokuja kuchezea Simba baadaye.
Miongoni mwa timu hizo ni Morning Stars, Canada Dry, Liverpool na Ilala Stuff, ambako huko mchezaji aliyeonekana kukomaa alipelekwa kukipiga Sunderland.
Majina Maarufu
Zaidi ya jina la Simba, kama zilivyo timu nyingine maarufu duniani, timu hii pia hutambulika kwa majina mengine tofauti.
Hufahamika pia kwa jina la Wekundu wa Msimbazi, Taifa Kubwa na Lunyasi.
Jezi
Klabu ya Simba huvaa jezi nyekundu katika uwanja wake wa nyumbani na nyeupe inapokuwa ugenini. Wakati mwingine huvaa jezi zenye mchanganyiko wa rangi hizo mbili.
Uongozi
CHOMBO cha juu kabisa cha maamuzi katika klabu ya Simba ni Mkutano Mkuu wa Wanachama ambao ndiyo huchagua viongozi wa klabu.
Shughuli za kila siku husimamiwa na Kamati ya Utendaji ingawa sekretarieti ndiyo huzifanya kwa maelekezo ya kamati. Kiongozi wa Kamati ya Utendaji ni Mwenyekiti wa klabu na yeye pamoja na kamati yake yote inawajibika kwa wanachama moja kwa moja.
Safu ya Uongozi kwa Sasa
Mwenyekiti
Ismail Aden Rage
Makamu Mwenyekiti
Geofrey Nyange
Katibu Mkuu
Evodius Mtawala
Wajumbe wa Kamati ya Utendaji
Joseph Itang’are
Said Pamba
Daniel Manembe
Francis Waya
Sued Mkwabi
Ibrahim Masoud
Zakaria Hans Pope
NB: Kwa nyadhifa zao, Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Katibu Mkuu ni Wajumbe wa Kamati ya Utendaji kwa nyadhifa zao
MATAJI
KATIKA historia yake, Simba imetwaa jumla ya mataji 36, yakiwamo 17 ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara, katika michuano mbalimbali ambayo imeshiriki tangu ianzishwe.
Mataji hayo yanajumuisha ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Ligi ya Muungano, Kombe la Nyerere, Kagame na Kombe la Mapinduzi.
Haya Ndiyo Mataji Yaliyochulikuwa na Simba
UBINGWA WA LIGI KUU:
1965, 1966, 1973, 1976, 1977, 1978, 1979, 1980, 1984, 1990, 1994, 1995, 2001, 2003, 2004 na 2007 (Ligi Ndogo) na 2010.
LILILOKUWA KOMBE LA NYERERE:
1984, 1995 na 2000
LILILOKUWA KOMBE LA MUUNGANO:
1993, 1994, 1995, 2001, na 2002
KOMBE LA TUSKER:
2001, 2002, 2003 na 2005
KOMBE LA CAF:
Ilifika fainali mwaka 1993
KOMBE LA KAGAME:
1974, 1991, 1992, 1995, 1996 na 2002
LIGI YA MABINGWA AFRIKA:
Kucheza hatua ya makundi 2003
KLABU BINGWA AFRIKA:
Kucheza Nusu Fainali 1974
KWA TAARIFA ZAIDI TEMBELEA TOVUTI HII http://simba.co.tz/club-info
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment